KIKOSI cha Timu ya KMC FC kimeanzakufanya maandalizi kuelekea katika mchezo wake dhidi ya Namungo utakaopigwa siku ya Alhamisi Februali nne mwaka huu katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam saa 10.00 jioni.

Mchezo huo ni kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ya kuanza kuchezwa kwa mechi zilizoahirishwa (Viporo) ambapo KMC FC ni miongoni mwa Timu ambazo  mchezo wake dhidi ya  Namungo uliahirishwa.

Aidha hadi sasa maandalizi ya mchezo huo yanaendelea vizuri chini ya Kocha Mkuu John Simkoko pamoja na msaidizi wake Habibu Kondo na kwamba mpango mkakati ni kuhakikisha kuwa KMC FC  inafanya maandalizi ya kutosha na hivyo kuondoka na alama tatu muhimu dhidi ya wapinzani  Namungo FC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...