Mchezo huo ni kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ya kuanza kuchezwa kwa mechi zilizoahirishwa (Viporo) ambapo KMC FC ni miongoni mwa Timu ambazo mchezo wake dhidi ya Namungo uliahirishwa.
Aidha hadi sasa maandalizi ya mchezo huo yanaendelea vizuri chini ya Kocha Mkuu John Simkoko pamoja na msaidizi wake Habibu Kondo na kwamba mpango mkakati ni kuhakikisha kuwa KMC FC inafanya maandalizi ya kutosha na hivyo kuondoka na alama tatu muhimu dhidi ya wapinzani Namungo FC.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...