Maofisa wanaofanya kazi katika maeneo ya ukaguzi wa  mizigo kwa kutumia mionzi wakiangalia namna mzigo unavyopita katika mashine ya ukaguzi kabla ya kuruhusu kwa mionzi.

Mratibu wa mafunzo ya kozi ya kitaifa ya ukaguzi wa mizigo kwa kutumia mionzi Bwana Atumaini Makoba akiwaelekeza maofisa walioko kwenye mafunzo hayo kifaa cha kupima mionzi wakati wa kufanya ukaguzi wa mizigo.

Maofisa  wanaofanya mafunzo ya kitaifa ya ukaguzi wa mizigo kwa kutumia mionzi , wakioneshwa namna chanzo cha mionzi inapotokea ili kuweza kutambua  sehemu ya kukaa wakati mashine inafanya kazi  kwa ajili ya kujilinda na athari zitokanazo na mionzi.

 Na Mwandishi wetu, Arusha

WAFANYAKAZI  wanaofanya kazi ya kukagua  mizigo na bidhaa mbali mbali za wageni  wa ndani na nje ambao wako kwenye kozi ya kitaifa ya ukaguzi wa mizigo kwa kutumia mionzi inayondeshwa na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) yenye makao makuu yake jijini Arusha, jana wamefanya mafuzo hayo kwa vitendo katika maeneo ya viwanja vya ndege, maabara za Tume na  katika hoteli.

Mratibu wa mafunzo hayo wa Tume ya Nguvu za Atomiki (TAEC) Atumaini Makoba amesema mafunzo kwa vitendo yanasaidia  maeneo ambayo mionzi  inapotoka kwenye mashine za ukaguzi wa mizigo ili waweze kupunguza wingo wa mionzi wanayopata pasipo lazima kwa kukosa maarifa ya mahala pazuri pa kufanya kazi zao ili kujilinda madhara yanayoweza kujitokeza wakati wanafanya kazi zao.

“Hapa sasa tunawaonesha yale waliyosoma darasani kwa vitendo ili kuwapa ujuzi zaidi kwani itawasaidia kuepukana na madhara ya mionzi maana lazima anayepima mizigo afahamu kwa kina wapi mionzi inapotokea na inapoelekea wakati akifanya kazi hiyo”alisema Makoba wakati wa mafunzo hayo kwa vitendo.

Amesema katika kujifunza kwa vitendo ameona wapo baadhi ya wafanyakazi waliokuwa wakikosea katika utendaji wao wa kila siku, lakini baada ya kuwaonesha kwa vitendo wameweza kurekebisha pale walipokuwa wakifanya tofauti na kwamba sasa wana uhakika wataendelea kuzingatia usalama wa mionzi kwenye maeneo yao ya kazi  ili kujilinda na kuilinda jamii kwa ujumla.

Kwa upande wake kiongozi wa maofisa hao waliohudhuria mafunzo kwa vitendo  Bwana Lusajo  Masosi amesema mafunzo hayo ya vitendo yamewejengea uwezo wa namna ya kujilinda na athari za mionzi katika maeneo yao ya kazi.

Jumla ya maofisa 40 kutoka katika maeneo ya ujenzi wa miundombinu kama barabara na  mamlaka mbalimbali  kama vile viwanja vya ndege, hotelini, viwandani na bandarini wanashiriki mafunzo hayo ya matumizi salama ya teknolojia ya mionzi kwa siku tano hapa makao makuu ya TAEC-Arusha. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...