MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Machi 28,2021, imetoa angalizo la uwepo wa mvua kubwa kwa siku mbili kuanzia kesho Machi 29 na 30 mwaka huu katika mikoa

Katika taarifa iliyotolewa na TMA imeonyesha mvua hiyo yenye uwezekano wa wastani, itanyesha kesho Machi 29, kwenye baadhi ya maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani inayojumlisha Visiwa vya Mafia, Lindi, na Morogoro pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Aidha mvua hiyo inatarajiwa kunyesha kesho, Machi 30, kwenye baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, shinyanga, Kigoma, Katavi, Tabora, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Ruvuma pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro.

Athari zinazoweza kujitokeza ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji jambo linaloweza kuathiri shughuli za kiuchumi na ucheleweshwaji wa usafiri. Hata hivyo, TMA imewataka wananchi kuzingatia angalizo hilo.

Taarifa hiyo inayoelezea hali ya hewa kwa siku nne kuanzia Machi 29 imeonesha kuwepo kwa hali ya kawaida ya hewa kwa siku ya Machi 31 na Aprili Mosi, 2021.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...