NA FARIDA SAID,MORGORO.


Wakazi wa kata ya Mafisa Manispaa ya Morogoro wanalazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya nje ya kata hiyo kufuatia kituo cha afya cha Sina ambacho kingetatua changamoto hiyo baada ya kushindwa kukamilika kwa zaidi ya miaka 15 bila kumalizika kwa ujenzi wake mkoani hapa.
 
Wakizungumza wakati wa ziara ya Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM Morogoro Mjini katika kituo hicho mkoani hapa, walisema kuwa kituo hicho kimekuwa kikisuasua kutokana na kutokamilika kwa wakati jambo linalopelekea adha kwa wakazi wake kutembea umbali mrefu kufuata huduma bora za kiafya.
 
Sabrina Rajabu Mohamed alisema kuwa wakazi wa kata ya Mafisa wamekuwa wakipata adha kubwa ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya ikiwemo za mama na mtoto ambao hulazimika kutembea kufika katikati ya mji wa Manispaa ya Morogoro kusaka vituo cha afya.
Ametaja vituo hivyo ni pamoja na kituo cha Mwembesongo, Sabasaba, Nunge na Mfiga ambapo wamekuwa wakipata huduma za mama na mtoto.
 
“Endapo kituo cha afya Sina katika kata yetu hii ya Mafisa serikali ingekabilisha kwa wakati adha ya sisi ya kutembea umbali mrefu zingepungua lakini kwa sasa tunalazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya zaidi ya kilombeta tano hadi saba.”alisema Sabrina.
 
Diwani wa kata ya Mafisa, Joel Kisome alisema kuwa kutokana na adha wanayoipata wananchi wa kata hiyo ametoa kiasi cha sh45milioni kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa kituo hicho.“Nimetoa sh45milioni kama sehemu ya mchango wangu wa kuchangia maendeleo katika kata hii hasa katika kituo cha afya Sina lakini niiombe serikali kuongeza nguvu ili kituo hiki kiweze kukamika na kutoa huduma.”alisema Kisome.
 
Kisome alisema kuwa kukamilika kwa kituo hicho kitapunguza adha ya wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma za kiafya nje ya kata hiyo.
 
Alisema kuwa kukamilika kwa kituo hicho kutasaidia wananchi wa kata ya Mafisa kupata huduma karibu lakini na wananchi wa kata nyingine za jirani zikiwemo Tungi, Kihonda na Lukobe. 
Kwa upande wa Mwenyekiti huyo, Salumu Kapira alisema kuwa amefurahishwa na kitendo cha diwani wa kata hiyo kutoa fedha kumalizia baadhi ya mahitahi ya ujenzi huo.
 
Kapira amewatoa shaka wakazi wa kata ya Mafisa kuwa serikali imejipanga kumaliza kituo hicho cha Sina kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022 baada ya halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutenga sh50milioni.“Kazi iliyopo kwetu kama viongozi ni kusimamia miradi ya maendeleo lakini kuikumbusha serikali kwa ahadi ambazo zimetenga kwa ajili ya miradi fedha zinafika kwa wakati.”alisema Kipira.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...