Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limetoa kibali kwa Mabingwa wa Soka nchini, Simba SC kuingiza mashabiki 10000 katika mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya AS Vita ya DR Congo utakaopigwa Jumamosi ya April 3.
Awali CAF ilizuia Simba kuingiza mashabiki katika mechi zao za nyumbani kwa kisingizio cha hofu ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona hali iliyosababisha Simba icheze bila mashabiki kwenye mchezo wake uliopita dhidi ya El Merreikh ya Sudan ambapo Simba ilishinda kwa magoli 3-0.
Mchezo wa Jumamosi dhidi ya AS Vita ni muhimu kwa Simba kuweza kupata matokeo ya ushindi ama sare ili waweze kufuzu kwa hatua ya robo fainali. Kwa sasa Simba inaongoza kundi lao ikiwa na alama 10 ikifuatiwa na Al Ahly yenye alama saba huku AS Vita wenyewe wakiwa na alama nne na Merreikh wakiwa na alama moja.
Home
Unlabelled
NEWZ ALERT: CAF YAIRUHUSU SIMBA KUINGIZA MASHABIKI KWENYE MCHEZO WAO DHIDI YA AS VITA UWANJA WA TAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...