Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV - Dodoma

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema yeye sambamba na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli walikuwa kitu kimoja katika kutekeleza yale yote yaliahidiwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyokuwa ikinadiwa wakati wa Kampeni za Uchaguzi mwaka 2015 na 2020.

Akizungumza jijini Dodoma wakati akihutubia Bunge tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Samia amezishukuru awamu zote Tano za Uongozi katika mafanikio ya Taifa la Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika awamu zote Nane za Uongozi kwa kudumisha ustawi na maendeleo ya watu wa Zanzibar.

Aidha, Rais Samia amesema dira na muelekeo wa Serikali ya awamu ya Sita ni pamoja na kudumisha awamu zote zilizopita kwa kuendeleza yale yote mazuri na kuleta mengine mapya yatakayoleta tija kwa taifa la Tanzania.

Pia Rais Samia amewashukuru watangizi wake, akiwemo Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Amani Abeid Karume, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mtangulizi wake, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...