Charles James, Michuzi TV
KATIKA kuboresha sekta ya usafiri wa anga nchini, Serikali imepanga kulilea Shirika la Ndege kimkakati ili liweze kujiendesha na kukua lenyewe na kuweka mahesabu yake sawa.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Rais Samia Suluhu Hassan wakati akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo amesema katika kulilea Shirika hilo wamepanga kuliondolea tozo na madeni iliyonayo.
Rais Samia amesema Shirika hilo limekua likionekana halina thamani na linajiendesha kwa hasara kwa sababu ya kuwa na madeni mengi ambayo wamekua yakirithiwa kwa muda mrefu.
" Kwa sasa Shirika letu linaonekana halina thamani kwa kuwa limethiri madeni mengi ya nyuma, hatutokubali kuona shirika letu linapata hasara ilihali tumelifanyia Uwekezaji mkubwa.
Tunaenda kufanya uchambuzi wa kina kuona namna gani ya kuliendesha kwa faida Shirika letu kwa kuwa na rasilimali watu bora tena tuliowachunguza na kuwaamini," Amesema Rais Samia.
Akizungumzia sekta ya Utalii, Rais Samia amesema serikali ya awamu ya sita imepanga kuwekeza katika Utalii wa mikutano, fukwe na malikale lengo likiwa ni kuongeza idadi ya watalii watakaotembelea vivutio vyetu nchini pamoja na mapato ya sekta hiyo kutoka Sh Bilioni 2.6 hadi Bilioni Sita.
" Katika kukuza sekta hii pia tumepanga kuwahamasisha wawekezaji kuwekeza kwenye sekta hii kwa kujenga mahoteli na pia kama serikali kusomesha vijana wetu ili kupunguza kutegemea wataalamu kutoka nje ya Nchi, " Amesema Rais Samia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...