Charles James, Miçhuzi TV

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amemshukuru Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini katika serikali yake na kumuahidi kuendelea kuitumikia nafasi hiyo akifuata maelekezo yake kwa weledi mkubwa.

Majaliwa amesema ni jambo la kumshukuru Rais kwa kumuamini katika nafasi hiyo ya uwaziri mkuu licha ya jana kufanya mabadiliko madogo kwenye baraza la mawaziri.

Waziri Mkuu Majaliwa ametumia nafasi hiyo kumpongeza Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Katanga akimsifu kwa namna ambavyo amekua akifanya kazi kwa uaminifu na mafanikio kwenye nafasi zote alizowahi kuzishika.

" Nimpongeze sana Balozi Katanga namfahamu vizuri sana amekua Katibu Mkuu wangu nikiwa Tamisemi, nimhakikishie ushirikiano, na kwa mawaziri wenzangu tunaahidi kwako Rais kuwa tupo tayari kuwatumikia watanzania.

Tukuahidi kwamba tutaendelea kukupa heshima na kutunza uaminifu wako kwetu tukifanya kazi kwa uweledi lengo likiwa kutekeleza ahadi za serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi katika kuwatumikia wananchi kwa asilimia 100," Amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...