RAWAN Dakik (20,) Mtanzania na kijana mdogo zaidi Afrika anayepanda mlima mrefu zaidi duniani amefanikiwa kupanda katika mzunguko wa pili na kufikia mita 7,200 usawa wa bahari leo bila uhitaji wa oksijeni.
Rawan atapumzika kwa siku tano katika kambi maalumu za mlima Everest kabla ya kuanza mzunguko wa mwisho wa kufikia mita 8,850, Rawan amesema;
'' Leo ilikua ngumu, nimehisi oksijeni imekua chini na kupelekea kasi upandaji wa mlima kuwa chini.'' Ameeleza Rawan ambaye pia alipimwa virusi vya Corona na kukutwa salama wakati akiendelea na upandaji wa mlima Everest.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...