Na Mwandishi Wetu

MSANII wa Muziki wa Kizazi Kipya Ali Kiba ameibua shangwe na nderemo katika  kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la clouds Mchongo.

Kilele cha onesho hilo kilifanyika kwenye uwanja wa michezo wa 'Business'uliopo Buza kwa Mama Kibonge.

Kiba aliibua shangwe hizo baada kupanda jukwaani na kuimba wimbo wake mpya wa 'Salute'.

Alipanda akiwa na kundi lake la madansa sambamba na  mdogo wake Abdul Kiba  na kuimba baadhi ya  nyimbo zake ikiwemo wimbo wake mpya unaofahamika kwa jina la 'Salute,Ndombolo ya solo.

Wakongwe wengine ni Chegge Chigunda kutoka TMK amekonga nyoyo za watu huku akifuatiwa na mkongwe wa dansi Muumin Mwinjuma ambaye aliimba wimbo wake 'Kwa Mpalange' ambao ndiyo anatamba nao hivi kwa hivi sasa.

Kundi la watangazaji wa Kipindi cha Leo Tena kinachorushwa na kituo hiko  kiliongoza jahazi la shughuli hiyo iliyodhaminiwa na DStv, majiko ya Moto Poa,Red Gold Tomato.

Aidha burudani zingine zilizojiri ni pamoja na  kinyang'anyiro cha kumpata  Miss Buza, pia wasanii mbalimbali ambao ni wazawa wa eneo hilo la Buza walipata nafasi ya kutoa burudani.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Ali Kiba pamoja wasanii wa Kundi lake la Kings Music Records wakitoa burudani katika  kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la clouds Mchongo
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Ali Kiba akitoa burudani ya nguvu katika  kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la clouds Mchongo
 Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Chege Chigunda akitoa burudani katika  kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la clouds Mchongo.
Mwanamuziki wa dansi, Muumini Mwinjuma akitoa burudani ya wimbo wa singeli uitwao kwa Mpalange katika  kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la clouds Mchongo.
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm  Jose Mara akitoa salamu kwa mashabiki wao wakati wa kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la Clouds Mchongo.

Mtangazaji wa redio ya Clouds Fm Gea Habibu akitoa salamu pamoja na kutambulisha kipindi chao kinachorushwa na radio hiyo wakati wa kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la Clouds Mchongo
Wasanii mbalimbali wakitoa burudani 
Msanii wa Maigizo, Bulton Mwemba ‘Mwijaku’ akiwa amembeba Miss Buza mara baada ya kutangaza kuwa Miss Buza wakati wa kilele Cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la Clouds Mchongo

Mambo ya uswazi hayo
Baadhi ya wananchi walioudhuria kwenye kilele cha onyesho la siku ya vibonzo lililoandaliwa na Clouds Media Groups linalofahamika kwa jina la clouds Mchongo



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...