Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango ameridhia na kuidhinisha matokeo ya watahiniwa 5,768  waliofanya mtihani kuanzia tarehe 4 hadi tarehe 7 Mei mwaka 2021 katika ngazi mbalimbali za masomo ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu  na Wakaguzi  wa Hesabu Tanzania (NBAA). Mitihani hiyo ilifanyika katika vituo 11 vya mitihani vilivyopo Tanzania Bara na Visiwani.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) CPA Pius  Maneno imebainisha kuwa matokeo hayo yanafuatia mitihani iliyofanyika katika vituo 11 vya mitihani kutoka mikoa kadhaa ya Tanzania Bara na Visiwani.

Alisema mitihani hiyo ilihusisha watahiniwa katika hatua ya kwanza na ya Pili katika ngazi ya cheti cha utunzaji wa  Hesabu (ATEC I , ATEC II) zenye masomo manne kila moja na ngazi ya taaluma, Hatua ya Awali/Msingi (Foundation Level) yenye masomo matano, Hatua ya Kati (intermiediate Level), yenye masomo sita na hatua ya mwisho yenye masomo manne.

"Watahiniwa  waliosajiliwa  walikuwa  6,401  kati ya hao watahiniwa   633  sawa na asilimia  9.9  hawakuweza  kufanya  mitihani  hiyo kwa sababu mbalimbali. Hivyo  watahiniwa   waliofanya   mitihani   walikuwa   5,768  sawa  na  asilimia

90.1. Kati ya watahiniwa hao 2,763 sawa na asilimia 47.9 ni wanawake na 3,005 sawa na asilimia 52.1 ni wanaume.

  Kati ya watahiniwa   waliofanya  mitihani  hiyo  watahiniwa   162 ambao ni asilimia 6.5  wamefaulu  mitihani  katika mkao mmoja, wengine  24 sawa na asilimia  0.7 wamefaulu  kwa  kufaulu  masomo  walioyokuwa   wameshindwa katika  mitihani  ya nyuma,  wengine  708  sawa  na  asilimia  12.5  wamefaulu mitihani  yao kwa  kufaulu  masomo  waliyokuwa   wamebakiza," alisema Maneno.   

Pia alisema  watahiniwa     894    sawa   na   asilimia    15.5   wamefaulu    mitihani    yao na kwamba watahiniwa   wengine   2,624  sawa  na  asilimia   45.5  wamefaulu   baadhi  ya masomo  katika  ngazi  mbalimbali  na watahiniwa  2,250  waliobakia   sawa na asilimia  39.0 hawakufaulu  mitibani  yao.

Awali, taarifa hiyo ilieleza kuwa watahiniwa waliosajiliwa    walikuwa   709  kati  ya  hao watahiniwa   60  sawa na asilimia  8.5 hawakuweza   kufanya  mitihani hiyo kwa  sababu  mbalimbali na hivyo kufanya ndani ya watahiniwa   waliofanya  mitihani kuwa  649   sawa  na  asilimia   91.5.     

Pia imeelezwa kuwa kati   ya  watahiniwa  649 waliofanya  mitihani katika ngazi hii watahiniwa  95  ambao ni asilimia

14.6  wamefaulu   mitihani  katika  mkao  mmoja huku wengine  02  sawa  na asilimia   0.3  wamefaulu   masomo  waliyokuwa   wameshindwa  katika mitihani  ya nyuma,  wengine   112 sawa  na  asilimia  17.3  wamefaulu mitihani   yao  kwa  kufaulu   masomo   waliyokuwa   wamebakiza.   

Imeelezwa kwa ujumla watahiniwa  209  sawa na asilimia 32.2 wamefaulu  mitihani  yao na watahiniwa  312 sawa na asilimia  48.1 wamefaulu  baadhi  ya masomo katika  ngazi  hii.  Watahiniwa   128  waliobakia   sawa  na  asilimia   19.7 hawakufaulu  mitihani  yao.

Aidha, katika hatua ya  Kati, waliojisaliwa walikuwa   3,275   kati  ya  hao watahiniwa  379 sawa na asilimia 11.6 hawakuweza   kufanya  mitihani kutokana na sababu  mbalimbali. Hivyo watahiniwa  waliofanya  mitihani walikuwa 2,896 sawa na asilimia 88.4.   Kati ya watahiniwa 2,896 waliofanya  mitihani  katika ngazi hii  watahiniwa   28 ambao ni asilimia

1.0  wamefaulu   mitihani   katika  mkao  mmoja,   wengine  19  sawa  na asilimia     0.7     wamefaulu     kwa     kufaulu     masomo waliyokuwa wameshindwa    katika   mitihani  ya  nyuma.

Alisisitiza kuwa wengine 302 sawa na asilimia    10.4   wamefaulu     mitihani yao kwa kufaulu    masomo waliyokuwa    wamebakiza, hivyo  Kwa   ujumla   watahiniwa    349  sawa   na asilimia   12.0  wamefaulu   mitihani   yao.  Watahiniwa   1,372  sawa  na asilimia    47.4   wamefaulu baadhi  ya masomo    katika    ngazi   hii. Watahiniwa    1,175  waliobakia   sawa  na  asilimia   40.6  hawakufaulu mitihani  yao.

Katika hatua ya mwisho, waliosajiliwa walikuwa 2,159 kati ya hao watahiniwa 181 sawa na asilimia 8.4 hawakuweza kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali. Hivyo watahiniwa waliofanua mitihani walikuwa 1,978 sawa na asilimia 91.6. Kati ya watahiniwa 1,978 waliofanya mitihani katika ngazi hii watahiniwa 21 sawa na asilimia 1.1 wamefaulu mitihani katika mkao mmoja, mwingine 01 sawa na asilimia 0.1 amefaulu kwa kufaulu masomo aliyokuwa ameshindwa katika mitihani ya nyuma.

Amesema watahiniwa    268  sawa   na asilimia   13.5  wamefaulu   mitihani   yao.  Watahiniwa    832  sawa  na asilimia    42.0  wamefaulu    baadhi    ya   masomo    katika   ngazi   hii. Watahiniwa    856   waliobakia    sawa   na   asilimia   43.3   hawakufaulu mitihani  yao.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo ametoa pongezi kwa wale wote waliofuzu mitihani yao na kuwataka wale ambao hawajafuzu kutokata taama badala yake waongeze bidii zaidi katika masomo yao ili wawezo kufuzu mitihani ijayo.

 

BOFYA HAPA KUYATAZAMA MATOKEO HAYO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...