Na Mwamvua Mwinyi, Kibiti
Wananchi
wameaswa kushirikiana na TAKUKURU ,kupambana na rushwa na kufichua
waomba rushwa ambao uomba rushwa wakati wa kutoa huduma mbalimbali za
kijamii ili waweze kuchukuliwa hatua.
Aidha
idara na taasisi zinazotoa huduma kwa jamii ikiwemo Jeshi la polisi
kitengo cha usalama barabarani, hospital zimeelekezwa kukusanya mapato
kwa njia ya kielektroniki, TEHAMA ili kuongeza pato la Taifa na
kurahisisha huduma.
Akitoa
ujumbe wa mwenge wa uhuru kwa wananchi wa Rufiji pamoja na kuzindua
klabu ya kupambana na rushwa shule ya sekondari Mahege,mkoani Pwani,
Kiongozi wa mbio za mwenge maalum ,L.T Josephine Mwambashi alisema,
jamii itambue mapambano hayo sio jukumu la TAKUKURU pekee.
Mwambashi alielezea, rushwa inarudisha nyuma maendeleo.
Hata
hivyo , akielezea umuhimu wa TEHAMA aliwataka wanafunzi kutumia njia
hiyo ikiwemo simu, komputa ,Tv kuongeza uelewa na ufahamu wa mambo ya
masomo lakini sio kwa kumong'onyoa maadili yetu.
Akiweka
jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa miundombinu ya maji safi katika
Kijiji cha Nyamisati ,unaosimamiwa na wakala wa maji na usafi wa
mazingira vijijini (RUWASA ), Mwambashi alisema wanaosimamia miradi
wahakikishe wanashirikisha jamii ili itambue.
Mradi
mwingine ni Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya
walimu katika shule ya sekondari Zimbwini, Mwambashi alipokea taarifa ya
mradi iliyosomwa na mkuu wa shule hiyo Estomic Kimwemwe ambapo
alielezea ,malengo ya mradi ni kupunguza msongamano wa wanafunzi
madarasani.
Alisema
,utekelezaji wa mradi ulianza mei 2021 na ulitarajiwa kukamilika agost
20 ,mwaka huu fedha zilipokelewa kwa ajili ya Ujenzi zimetumika milioni
39.662.5 na zimebakia 337,500 .
Awali
akipokea mbio maalum za mwenge wa uhuru ,kutokea wilayani Rufiji,mkuu
wa wilaya ya Kibiti ,kanal Ahmed Abbas Ahmed alisema ,mwenge huo
utatembelea miradi 15 yenye thamani ya sh .474.540.5.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...