Na Mwamvua Mwinyi, Kibiti


Wananchi wameaswa kushirikiana na TAKUKURU ,kupambana na rushwa na kufichua waomba rushwa ambao uomba rushwa wakati wa kutoa huduma mbalimbali za kijamii ili waweze kuchukuliwa hatua.

Aidha idara na taasisi zinazotoa huduma kwa jamii ikiwemo Jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani, hospital zimeelekezwa kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki, TEHAMA ili kuongeza pato la Taifa na kurahisisha huduma.

Akitoa ujumbe wa mwenge wa uhuru kwa wananchi wa Rufiji pamoja na kuzindua  klabu ya kupambana na rushwa shule ya sekondari Mahege,mkoani Pwani, Kiongozi wa mbio za mwenge maalum ,L.T Josephine Mwambashi alisema,  jamii itambue mapambano hayo sio jukumu la TAKUKURU pekee.

Mwambashi alielezea, rushwa inarudisha nyuma maendeleo.

Hata hivyo , akielezea umuhimu wa TEHAMA aliwataka wanafunzi kutumia njia hiyo ikiwemo simu, komputa ,Tv kuongeza uelewa na ufahamu wa mambo ya masomo lakini sio kwa kumong'onyoa maadili yetu.

Akiweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa miundombinu ya maji safi katika Kijiji cha Nyamisati ,unaosimamiwa  na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA ), Mwambashi alisema wanaosimamia miradi wahakikishe wanashirikisha jamii ili itambue.

Mradi mwingine ni Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu katika shule ya sekondari Zimbwini, Mwambashi alipokea taarifa ya mradi iliyosomwa na mkuu wa shule hiyo Estomic Kimwemwe ambapo alielezea ,malengo ya mradi ni kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani.

Alisema ,utekelezaji wa mradi ulianza mei 2021 na ulitarajiwa kukamilika agost 20 ,mwaka huu fedha zilipokelewa kwa ajili ya Ujenzi zimetumika milioni 39.662.5 na zimebakia 337,500 .

Awali akipokea mbio maalum za mwenge wa uhuru ,kutokea wilayani Rufiji,mkuu wa wilaya ya Kibiti ,kanal Ahmed Abbas Ahmed alisema ,mwenge huo utatembelea miradi 15 yenye thamani ya sh .474.540.5.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...