Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa akifafanua jambo wakati wa mkutano na wadau wa Mkoa wa Dodoma wa kuhamasisha na kutoa elimu juu ya sensa ya watu na makazi.


Na Richard Mwaikenda, CCM Blog Dodoma


KARANI yeyote wa Sensa atakayetoa siri  ya mtu wakati wa Sensa ya Watu na Makazi atashitakiwa na kuhukumiwa kulipa sh. mil. 10 au kufungwa miaka miwili ama vyote kwa pamoja.

Adhabu hiyo imeelezwa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa wakati wa mkutano na wadau wa Mkoa wa Dodoma wa kuhamasisha na kutoa elimu juu ya sensa ya watu na makazi.

"Uzuri sheria iko wazi kwa kosa hilo, hivyo si vizuri kwa karani wa sensa ambaye amepewa mafunzo yakiwemo ya maadili ya kutunza siri za anaowahoji halafu akafanya vinginevyo," amesema Dkt. Chuwa.

Dkt. Chuwa ameamua kujibu hivyo baada  mmoja wa wadau wa mkutano huo, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Mkoa wa Dodoma, Mchungaji Petro Mpolo kuelezea hofu waliyonayo kwa baadhi ya makarani wa sensa kutoa siri walizohojiwa jambo ambalo alidai linasababisha  wengi wao kusita kueleza ukweli.

Mkutano huo wa wadau ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa ya Mkoa huo, Anthony Mtaka ulihudhuriwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Wengine ni Kamishna wa Sensa, Spika mstaafu, Anne Makinda, wabunge wa mkoa huo, wakuu wa wilaya, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa mabaraza ya wazee na taasisi mbalimbali wakiwemo watu wenye ulemavu.

Sensa ya Watu na Makazi itafanyika Agosti 2022 ambapo uzinduzi utafanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Makao Makuu ya Nchi Dodoma.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...