Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetenga takribani shilingi bilioni 41.87 kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini mkoani Rukwa.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani leo Agosti 26, 2021 alipokuwa akizindua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa  pili katika kijiji cha Lowe kata ya Lusaka Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa.

Fedha hizo zitatekeleza miradi ya umeme kwenye vijiji  339 katika mkoa wa Rukwa.

Aidha, Dkt. Kalemani amesema kuwa, Serikali imetenga jumla ya shilingi Trilioni 1.24. kwa ajili ya kukamilisha utekelezaji  wa miradi ya umeme Vijijini awamu ya tatu  mzunguko wa pili hadi kufikia mwezi septemba mwaka 2022.

"Tanzania imefikia asilimia 86 ya usambazaji wa umeme katika vijiji na kuifanya kuwa ya kwanza Afrika kwa kusambaza umeme vijijini" alieleza Dkt. Kalemani.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...