Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Othman Masoud Othman, amewasihi
Waislamu nchini kurudi katika mila, desturi na kufuata sheria za dini
ili kutunza haiba na sifa za Zanzibar kote ulimwenguni.
Ameyasema
hayo mara baada ya kumaliza ibada ya Sala ya Ijumaa katika Masjid
Shifaa uliopo Michenzani Mjini Unguja, ambapo amesisitiza kuwa kuna
mambo mengi yaliyokuwa yakifanywa na wazee wetu walioishi nchini
zikiwemo mila na desturi zinazoendana na miongozo ya dini ya Kiislamu
ambayo yaliipa heshima kubwa Zanzibar.
“Zamani
wageni waliokuwa wakitembelea hapa walikuwa wakiishi kupitia mila na
silka zetu na hilo ndilo lililoifanya Zanzibar kupata umaarufu”, amesema
akiongeza kwamba hayo ni mambo ya kudumishwa ili Zanzibar irudi katika
hadhi na haiba yake.
Alhaj
Othman amekumbusha kuwa hapa Zanzibar kuna mambo mengi yamefanywa na
watawala wa Kiingereza kama vile kuanzisha mahakama ya kadhi, kamisheni
ya wakfu na kuongoza nchi kwa sheria ya Kiislamu kutokana na kukuta kuwa
nchi hii ilikuwa na misingi ya dini na mila bora kabisa.
"Kama
tutafuata vyema miongozo ya dini, basi jamii zetu zitakuwa na upendo na
kuheshimiana sana jambo litakaloondoa hata vitendo vya kihalifu"
alisisitiza Makamu huyo wa kwanza wa Rais.
Mapema
khatibu wa msikiti huo, Sheikh Ahmed Muumin, amewahimiza Waislamu hao
kuutumia muda wao katika kufanya amali njema kwa lengo la kujitengenezea
maisha bora kwa Mwenyezi Mungu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...