Na Amiri Kilagalila,Njombe


Kesi za utelekezaji,ulawiti,ubakaji na unyanyasaji wa kingono umetajwa kuongeza kiwango cha ukatili katika halmashauri ya wilaya ya Njombe hadi kufikisha matukio ya ukatili wa kijinsia 161 katika kipindi cha miaka miwili ya 2019/2020 na 2020/2021.

Taarifa hiyo imebainishwa na afisa ustawi wa jamii halmashauri ya wilaya ya Njombe Avelino Chaula kabla ya mkutano wa baraza la madiwani wa halmashauri hiyo uliofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari Mtwango na kulazimika kutoa  elimu kwa madiwani na wajumbe wa baraza hilo juu ya ulinzi na usalama wa mtoto kwa madiwani na maofisa watendaji wa kata na kwamba katika matukio hayo yote lakini matukio ya utelekezaji yameripotiwa mengi zaidi kuliko mengine.

“Kwa miaka miwili tuna matukio 161 lakini matukio yanayoongoza kwa wingi ni ya utelekezaji na ukiangalia matukio ya utelekezaji kwa mwaka wa kwanza tuna matukio 42,na mwaka wa fedha 2020,2021 tuna matukio 57 na haya ni kwa yale yaliyotufikia ofisini sasa tujiulize ni mangapi hayajafika?tuombe wazazi wawajibike kulea watoto”alisema Chaula

Kutokana na hali hiyo baadhi ya madiwani wa kata mbalimbali akiwemo  Neema Mbanga, Isaya Myamba na Roida Wandelage wametaka kuwekwa kwa mikakati maalumu ya kushughulikia changamoto za ukatili ikiwemo tatizo la kesi nyingi za ujauzito wa watoto kutomalizika.

“Watoto wengi wanapita mimba lakini ukianza kufuatilia unaona tu imeishia hewani kwa hiyo ninaomba halmashauri tuweze kuwa makini na kuyafuatilia haya kwa nguvu zote”alisema Neema Mbanga 

“Nadhani kuna sababu ya msingi ya kujipanga upya namna ya kudhibiti na kushughulikia kesi hizi kuhakikisha zinaisha”Alisema Isaya Myamba

Naye Roida Wandelage alisema “Mtaani kuna kawaida ya kusema kipi bora nimfunge yule ambaye amempa mtoto mimba au nimuache anilelee mtoto wangu na haya wanayafahamu”

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Njombe George Makacha ambaye ni mwanasheria na Valentino Hongoli ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo wamewataka madiwani na maofisa watendaji kuitumia mikutano yao ya hadhara kuhakikisha wanatoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia katika jamii.

“Sheria inataka kama motto amepewa mimba lazima sheria zichukuliwe na sisi kama viongozi ni vema tutoe elimu zaidi ili wazazi waelimike na kuona uchungu juu ya watoto”alisema George Makacha

Valentino Hongoli alisema “Wakati mwingine sisi wenyewe tukijitathmini utakuta viongozi,watendaji na baadhi ya wananchi wanaonekana kioo kwenye jamii utakuta ni watelekezaji”

Katika ripoti ya afisa ustawi wa jamii   halmashauri hiyo kwa upande wa wanafunzi waliopata ujauzito ni 16 kwa mwaka 2020 na 18 kwa mwaka 2021.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Njombe Valentino hongoli wakati wa semina kwa viongozi na wajumbe wa baraza la madiwani akitoa wito kwa viongozi kuwa wakanza kupambana na vitendo vya ukatili ambavyo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikifanywa katika wilaya hiyo.
Afisa ustawi wa jamii halmashauri ya wilaya ya Njombe Avelino Chaula katika semina fupi kwa madiwani na viongozi akieleza idadi ya kesi zilizolipotiwa ndani ya wilaya hiyo zinazohusiana na maswala ya ukatili
:Baadhi ya wajumbe wa semina juu ya maswala ya ukatili na watoto wakimsikiliza afisa ustawi wa jamii akifundisha namna watoto wanavyotakiwa kulindwa pamoja kupambana na matendo ya ukatili.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...