Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
SERIKALI
kupitia wizara ya michezo pamoja na TFF imetakiwa kuangalia namna ya
kuinua suala la michezo makazini na kuandaa ligi maalum kati ya
watumishi wa Umma.
Akizungumza
katika mechi ya kirafiki baina ya TANROADS HQ (makao makuu )na TANROADS
-Pwani , katika bonanza lililoandaliwa na TANROADS Pwani ,mratibu wa
bonanza hilo ,Charles Ndyelabula alisema ,hatua hiyo itasaidia kuibua
vipaji vilivyojificha makazini.
"Michezo
hii inatuweka imara kufanya kazi ,mtumishi unakuwa na molari wa kutenda
kazi kwa bidii na afya inaimarika, Hata hii Corona wakati tunachoma
chanjo lakini pia tupende michezo inatupa afya njema"alifafanua Charles.
Katika mechi hiyo ,timu hizo zilitoka sare wakitoka wote suluhu ya bila bila.
Mchezaji wa HQ , Twahir Salim alieleza walijiandaa na kupata nafasi nyingi za wazi lakini hawakufanikiwa kushinda.
"Rais
,wizara ya michezo wangesisitiza michezo hii ,leo imenifunza kuwa
inajenga mahusiano ,tunajuana na kubadilishana mawazo ,tumefurahi
,Kifupi Tumeenjoy"!alisisitiza Salim.
Kwa
upande wake ,Asosa Mwanilwa ambae ni captain wa timu ya TANROADS Pwani
,alisema wamekubaliana na matokeo kwakuwa pande zote wamejitahidi.
Alisema
,kiukweli timu ya makao makuu ipo imara wanaonekana kuwa na mazoezi ya
kutosha hivyo wamejifunza ,sio kusubiri mabonanza ndipo wacheze bali
kila siku ni ya mazoezi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...