Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva Whozu ametunga wimbo maalum kwa ajili ya wanachama,mashabiki na wapenzi wa Klabu ya Simba ambao unakwenda kwa jina la Simba ni Noma.

Akizungumza leo Septemba 1,2021 Wohzu amesema ameamua kutunga wimbo huo kutokana na mapenzi yake makubwa na klabu ya Simba,yeye ni Simba kindakindaki,hivyo ameamua kutunga wimbo huo.

"Tunafahamiana wengi,mimi ni msanii wa muziki wa kizazi kipya,nimekuwa nikitumia talanta yangu katika sanaa ya muziki, hivyo nimeamua kitengeneza wimbo maaalum kwa ajili ya Simba,mashabiki wa Simba ,nimefanya hivyo kwasababu ya wachezaji wa Simba.

"Simba ni bingwa hata wasemeje, nimetumia ubunifu kidogo,sijaimba kwa Singeli bali nimechanganya ladha, nimetumia Singeli kidogo, bongo fleva kidogo na bolingo kidogo, nimechanganya ili kupata kitu kizuri, siko mwenyewe nimemshirikisha Donat Mwanza anayetokea Congo.

"Mwanamuziki huyo ameshawahi kuhiti na Bana Congo, ana wimbo wake ambao umekuwa maarufu sana. Lakini katika mazungumzo yangu na Donat Mwanza ni shabiki mkubwa wa Simba, hivyo haikuwa ngumu kumshawishi, kumshirikisha wimbo huo na tumeufanya kwa Kiswahili,Wimbo unaitwa Simba ni Noma.

"Simba ni  Noma, wimbo umerekodiwa na upo tayari wimbo ni mzuri sana na umeshatoka, wimbo huo ni maalum kwa ajili ya Simba, ni wimbo wa kushabikia Klabu, kokote uliko mwana Simba tembea kifua mbele,jidai wewe ni mshindi, kikubwa naipenda Simba ,ni Simba kindaki ndaki, tutauwimbo na mashabiki zetu, tutauumba kiubibgwa,amesema Wohzu.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Whozu akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 1,2021 jijini Dar es Salaam kuhusu wimbo wake maalum kwa ajili ya Simba ambao ameupa jina la Simba Noma

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...