Serikali imesitisha bei za mafuta zilizoanza kutumika leo kote nchini na kuunda timu ya kuchunguza na kuangalia viashiria vinavyofanya kupanda kwa bei.

Akizungumza katika viwanja vya Bunge leo, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), Godfrey Chibulunje amesema kila Jumatano ya mwisho wa mwezi Ewura hutangaza viwango vipya vya bei ya mafuta nchini.

Amesema kwa kuwa bei hiyo imeonekana kupanda na itaendelea kupanda, hivyo Serikali imeamua kuchukua hatua ya kusitisha ili bei zilizokuwa zinatumika mwezi uliopita (Agosti) ziendelee kutumika.

Chibulunje amesema Serikali imeunda timu maalum ya kuchunguza na kuangalia viashiria gani vinafanya bei kuongezeka.

Amesema baada ya timu hiyo kufanya kazi watarudi tena kwa wananhi kutoa maelekezo maalum.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...