Raisa Said, Lushoto.


Mkuu wa Wilaya ya Lushoto  Mkoani Tanga Kalisti Lazaro  amewataka  Wazazi  na Walezi   kutokuwaacha  vijana  wao  nyumbani  wanapomaliza  elimu  ya msingi  na sekondari  na badala yake  wawaendeleze kielimu  ili waweze kubobea  kitaaluma  katika  karne hii ya Sayansi  na teknorojia .

Pia amewataka  Wazazi  hao  kuacha  mara moja tabia  yakuwarubuni  Watoto  wao kufanya  vibaya  katika mitihani yao  ya kitaifa  kwa lengo  la kwenda kufanya kazi za  ndani [UYAYA} ili wao  wajipatie kipato.

Wito  huo  ameutoa  wakati  wa mkutano wa hadhara  uliofanyika  kata  ya Mbwei  wilayani  humo ambako  kwa miaka  mitatu  mfululizo  shule tatu za msingi zilizopo katika kata hiyo zimeshika nafasi ya mwisho katika mitihani ya kumaliza darasa la Saba.

"Sasa hivi kuna janga la corona lakini Katika kata hii kunajanga la kuferi hii ni aibu kubwa  tubadilike tusiwarubuni watoto wetu kufanya vibaya mitihani yao ili wakafanye uyaya  Mombasa,Tanga,Dar Es Salaam na Arusha" Alisema Mkuu hiyo wa Wilaya.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa  watoto  ni taifa  la kesho hivyo wanatakiwa kujengewa  mazingira  mazuri ili waweze kutimiza ndoto zao  za badae badala ya kuruhusu kwenda kufanya kazi za ndani kwa watu.

"Ndugu zangu hamkuzaa ili watoto wenu waende kufanya kazi za ndani kwa watu  acheni mara moja tabia hiyo ya kuwaambia watoto wafanye vibaya mitihani yao kabla hatua Kali zakisheria hajizachukuliwa kwa wazazi wote watakaobainika kufanya hivyo" Alisisitiza

Aliongeza kuwa inasikitisha Sana kuona watoto wanafeli lakini shule zinashika nafasi ya mwisho hii ni aibu kubwa na haikubaliki Katika Wilaya hii,alitolea mfano kwa mwaka 2019  shule ya msingi  Mbwei Wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 142 na waliofauli walikuwa tisa na kwa mwaka 2020 waliofanya mtihani walikuwa  91 waliofauli ni wanne .

Kwa upande wa  shule ya Mavului  kwa mwaka jana walifanya mtihani walikuwa  45 waliofauli kwenda sekondari  walikuwa wa wili na kwa shule ya Mhezi kwa walifanya mtihani mwak jana walifanya mtihani walikuwa 95 waliofaulu walikuwa tisa.

Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza kuwa enzi za kufelisha zilishapitwa na wakati" Mimi nimemaliza elimu ya msingi mwaka 1990 tukafaulu watu watano wengine walikosa shule sababu hakukuwa na shule za kata lakini hivi Sasa  shule zipo nyingi hivyo mnatakiwa mfaulishe watoto wengi Kwakuwa shule zipo na Rais anatopesa kila shule ambapo kila shule inapata laki tano kwa mwezi na kwa mwaka milion sita" Alisisiza Lazaro.

Lazaro alisema kuwa Rais Samia kila mwezi amekuwa akitoa  sh.Laki tano kila shule ili watoto wasichangishwe wapewe elimu bure ambapo kila shule kwa mwaka inapewa mili.sita.

Pia alitumia fursa hiyo kuwahimiza Wazazi kuchangia chakula shuleni sababu chakula kinaongeza ufaulu

Nae Mbunge wa Jimbo hilo Shabani Shekilindi Maarufu Bosnia alisema kwa miaka mitatu mfululizo shule hizo zinaferisha lakini walifanya utafiti wakagundua Kuna wazazi wanawarubuni watoto  wao wafanye vibaya mitihani yao sababu walimu wanadai  watoto darasani wako vizuri lakini kwenye mitihani yao ya kumaliza elimu yao ya msingi  ndo wanafanya vibaya.

Shekilindi alisema kuwa  kunabaadhi ya wazazi wamewafanya watoto wao kitega uchumi sababu kila  mwezi watoto  waliopo mijini kufanya kazi za ndani uyaya huwa wanawatumia wazazi wao shilingi elfu 20 hadi 30 baad ya kupewa mshahara yao kila mwezi.

Zitta Thomas ni Mwalimu Mkuu Shule ya msingi Mbwei alisema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni mlundikano wa Wanafunzi katika darasa moja  hivyo ametupa kilio chake kwa serikali kuona umuhimu was kuongeza shule nyingine ili kuwapa nafasi walimu kufundisha kwa weledi na Wanafunzi kuelewa kwa ufasaha.

Mwalimu huyo pia alisema muamko mdogo wa elimu Katika kata hiyo ni sababu Kuna wazazi hawaelewi umuhimu wa elimu hivyo ameiomba serikali itunge sheria za kukomesha tabia ili kuwa nusuru watoto wanamaliza elimu yao .

Nuru Mdimu ni  Mzazi na Mkazi wa kata Mbwei  alisema sio kweli kwamba wanawarubuni watoto woa kufanya vibaya katika mitihani  yao nakwamba yeye changamoto kubwa anayoiona inasabaisha watoto kufanya vibaya ni wingi was wanafunziuliopo Katika shule hizo.

Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Lushoto  Emanueli Vuli  alisema kutokana na changamoto hiyo wameanza mikakati kwaajili ya kuongeza ufaulu kwa kuongeza walimu  pamoja na kuanza mkakati wa kugawanya  shule hiyo lengo kuboresha elimu Katika kata hiyo .






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...