Raisa Said,Muheza

Mkuu wa Wilaya ya Muheza  Mkoani Tanga  Halima Bulembo  amesema Wilaya hiyo imetengewa kiasi cha fedha sh.1.5  Bilioni za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19. 

Hayo aliyasema wakati Akizungumza na Wananchi wa  Tarafa ya Bwembela Wilayani humo  ambapo  alisema Fedha hizo ni  sehemu ya  1.3  trilion zilizotolewa na serikali hivi karibuni.

 Mkuu huyo wa Wilaya Bulembo alisema fedha hizo walizotengewa zinakwenda kumaliza changamoto mbalimbali  ikiwemo ya  upungufu wa madarasa, bweni na madarasa 10 ya shule Shikizi  na hivyo kufanya wanafunzi watakaojiunga na kidato cha Kwanza na wale wa Shule shikizi kuondokana na changamoto hiyo.

"Tunaishukuru  Serikali ya Rais Mama Samia  kwa kutupatia wana Muheza fedha hizo.  kwa ajili ya Ujenzi wa madarasa 57, ujenzi wa vituo vitatu vya shule shikizi vyenye madarasa 10, ujenzi  bweni moja la Wanafunzi wenye mahitaji maalum, na ujezi wa  vyumba vya  huduma za wagonjwa mahututi ( ICU) " Alisema Bulembo.

Akitoa mchanganuo  wa fedha alisema kwenye ujenzi wa ICU wametengewa sh milion 100 huku bweni la Wanafunzi wenye mahitaji maalum likitengewa sh.milion 80.

Kwenye Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa kwa Shule za Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Muheza imepatiwa Vyumba 57 vya Madarasa kwa shilingi Milion  20  kwa chumba kimoja hivyo kufikia . 1.1 bilion

katika  vyumba vya madarasa  vitakavyojengwa katika  vituo shikizi  vimetengewa  sh.miion 200,000,000




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...