Na.Vero Ignatus,Arusha

Wataalam wa wanayofanya kazi karibia ana mionzi wamepatiwa mafunzo maalum ili kujikinga na madhara yanayotokana na athari za mionzi 

Akizungumza mkuu wa Idara ya uhifadhi ya mabaki ya vyanzo vya mionzi mwishoni mwa Juma Jijini ArushaSalehe Mulisha   ambae amemuwakilisha mkurugenzi mkuu wa TAEC aliwataka kutumia mafunzo hayo kujikinga na athari zitokanazo na mionzi

Amesema lengo kubwa ni kuwakumbusha Usalama wa kazi katika maeneo yenye vyanzo vya mionzi ,ambapo mafunzo hayo yanatoa Elimu ya kujikinga na Mionzi, kwani kufanya kazi bila kuzingatia Usalama ,kunaweza kuleta madhara makubwa kwa anaetumia sambamba na kwa wagonjwa wanaotumia

"Haya ni mafunzo muhimu Sana kwasababu tulikuwa tunajaribu kuwakumbusha wenzetu umuhimu wa kuzingatia masuala ya usalama wakati wa kufanya kazi na vyanzo vya mionzi"Alisema Salehe

Nae Mratibu wa mafunzo hayo ambae pia ni mtafiti katika Tume ya Nguvu ya Atomic Wilbroad Mlogora (TAEC ) anamsema mafunzo hayo yanalenga kuinua uelewa wa Kinga  ya mionzi kwa wafanyakazi, ambao wanafanya kazi kwenye Tiba kwa njia ya X-Ray,kwani wao nitofauti na wafanyakazi wengine,kwani wao na mgonjwa wanakuwa chumba kimoja, hivyo upo uwezekano mkubwa Kama wasipopata mafunzo ya namna ya kujikinga wakapata madhara.

Kwa kuzingatia hayo madhara yanaweza kuepukika ,Ila kupata mionzi hakuwezi kuepukika ,kwani inafahamika kila kitu kina madhara na faida zake,hivyo wanao  uhakika kutokana na mafunzo hiyo mionzi kidogo wanayoipata, haitaweza kuwaletea madhara .

Kwa upande wa washiriki wa mafunzo hayo Idrisa Juma kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete,ambae ni Afisa mteknolojia wa Elimu ya mionzi , alisema   kuwa kutokana na Elimu waliyopatiwa imezidi kuwaongezea weledi na ufanisi katika ufanyaji wa kazi, kwasababu huwa wanaendesha mitambo ya mionzi katika tiba na katika upimaji,hivyo itawasaidia kuwakinga wengine dhidi ya mionzi 

 Martha Emmanuel Mbona yeye ni muuguzi kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete,anasema yeye anafanya kazi katika chumba ambacho wanatumia mionzi na wanashughulika na utambuzi, uchunguzi wa mishipa ya damu ya Moyo pamoja nakuziba matundu madogo ya Moyo haswa kwa watoto na watu wazima

Hivyo Mafunzo hayo yatawasaidia katika utendaji wao wa kazi kwani yeye ni mtu wa pili kutoka kwa Daktari ,hivyo itamsaidia kujilinda na mionzi kwasababu wanapoendelea na kazi katika chumba wanakuwa pamoja na mgonjwa, hivyo Ile mionzi anayoioata mgonjwa anategemea itanipata japo kwa kiasi kidogo,kwani mafunzo aliyoyapata yatamsaidia jinsi gani itapungiza Ile dozi  iwe kwenye dozi ndogo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...