Na Khadija Kalili, Kibaha
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa  Pwani RPC Wankyo Nyigesa ametoa amri kwa wakazi  wa Mkoa wa Pwani kwa Kila anayemiliki silaha  kinyume  cha sheria  aisalimishe  silaha  yake  kwa hiari  katika  vituo  vilivyo karibu  ikiwa ni pamoja na  Ofisi za serikali za mtaa, Ofisi  za serikali  za vijiji  na Ofisi za Kata.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa habari  leo alisema kuwa  zoezi hilo lilianza Novemba mosi mwaka huu na litafikia tamati Novemba 30 na baada ya tarehe hiyo msako mkali utafanyika na atakaekaebainika  anamiliki silaha kinyume cha sheria  hatua kali zitachukuliwa.
RPC Wankyo alisema kuwa wamebaini kuwa kuna  baadhi ya Kampuni za ulinzi binafsi zinazotumia  silaha  zisizoruhusiwa kutumia silaha  zisizoruhusiwa kutumia katika ulinzi huku alizitaja baadhi ya silaha hizo kuwa ni gobole, rifle na short gun.
"Tunatoa  rai wamiliki wa Kampuni hizo wazihusishe  na kusajiri silaha zinazopendekezwa  ambazo ni shortgun  pump action na Kampuni itakayoshindwa  kuhuisha  silaha zake  itafutiwa usajili wa kumiliki Kampuni hizo"alisema RPC Wankyo.
Wakati huohuo RPC alisema kuwa wamefanya  msako katika Wilaya  Tano za Polisi Ili kudhibiti  na kuzuia  matukio mbalimbali ambapo pia wamekamata not bandia 108 (dola 100 Kila), simu 7 za aina mbalimbali, nyara za serikali meno ya tembo2, bangi Puli 13, kete 272 na kilo 172, gongo Lita 93.5, mifuko 20 ya saruji, Ndoo 6 za rangi ya maji, TV mbili aina ya A order, Kompyuta mpakato 1aina ya Toshiba.
Pia amewataka wananchi wote  wanaomiliki  vyombo vya moto  kupeleka kwenye ukaguzi katika vituo vya Polisi Ili vikaguliwe  ukaguzi huo inafanyika bure na baada ya ukaguzi muhusika atalupia stika  ya usalama barabarani  na kulipia sh.3000 gari ndogo na 5000 gari  kubwa,wiki ya nenda kwa  Novemba 21 mwaka huu.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...