Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewataka askari Polisi kutimiza wajibu wao kwa kutenda haki kwa wananchi wanaowahudumia na kuvitendea haki vyeo vipya walivyovipata kwa kuhakikisha wanatimiza na kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi.

IGP Sirro amesema hayo leo akiwa katika kambi ya medani ya kambapori iliyopo wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wakati akifunga mafunzo ya Kozi ya Uongozi Mdogo Ngazi ya Cheo cha Koplo wa Polisi ambapo jumla ya askari 1697 wamehitimu mafunzo hayo na kutunukiwa Cheo hicho cha KOPLO.

Naye Mkuu wa Shule ya Polisi Moshi SACP Ramadhan Mungi amesema shule hiyo ilipokea jumla ya wanafunzi 1712 na waliofanikiwa kuhitimu mafunzo hayo ni 1697 huku wengine 15 wakiachishwa mafunzo kutokana na sababu mbalimbali.

Aidha amesema mafunzo waliyopatuiwa yatasaidia kuwaongezea weledina maadili  na kupandisha viwango vyao vya uadilifu, uwaminifu, utii haki na uzalendo pamoja na kudumisha ukakamavu, ujasiri na nidhamu katika utendaji wa kazi zao za kila siku.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...