-Vodacom yaendelea kumwaga zawadi mbalimbali msimu huu wa sikukuu.


Mkuu wa Mauzo Vodacom Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Brigita Shirima (kushoto) akimkabidhi zawadi ya smart Tv mmoja kati ya washindi wa wiki ya tatu wa  promosheni ya " Show Love, Tule Shangwe” Geofrey Nyakuka (kulia) mkazi wa Tabata, katikati ni Masta Shangwe, jumla ya washindi sita walijishindia Tv za kisasa (Smart Tv) wengine sita simujanja (smartphone)  na washindi 50 walijishindia pesa taslimu. Ili uweze kushinda zawadi katika kipindi hiki cha sikukuu,  mteja wa Vodacom unatakiwa kununua bando au kutumia huduma ya M-Pesa kwa umpendae kwa kupiga *149 * 01#

Mkuu wa Mauzo Vodacom Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Brigita Shirima akizungumza na wakazi wa Tabata waliojitokeza kushuhudia promosheni ya msimu wa sikukuu ya "Show Love,Tule Shangwe" ambapo wateja wa Vodacom walijishindia zawadi mbalimbali wakiwa na wapendwa wao.




Mshindi wa zawadi ya simujanja(smartphone), Felix Deogratius (wapili kulia) akipokea zawadi yake ya simu kutoka kwa Mkuu wa Mauzo Vodacom Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Brigita Shirima kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika Tabata Muslim jijini Dar es Salaam, Wapili kushoto ni mama mzazi wa Deogratius nae alijipatia zawadi ya simujanja kutoka Vodacom. Promosheni hii inakuwezesha wewe na umpendae kupata zawadi, na ili ushinde mteja wa Vodacom unatakiwa kununua bando au kutumia huduma ya M-Pesa kwa umpendae kwa kupiga *149 * 01#

Kapu la Masta Shangwe lililosheheni vyakula mbalimbali lilitolewa kwa washindi ambao walijibu maswali kupitia EFM Radio.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...