Na Humphrey Shao, Michuzi Tv

SHIRIKA la nyumba la Taifa limekuja na mpango kabambe Kwa wateja wake ambao wanalimbikiza kodi Kwa kufunga vitasa vya kidigitali ambavyo  vitakuwa vinajifunga venyewe (Automatic) hivyo mpangaji kushindwa kuingia ndani wala kutoka nje.

Akizungumza hayo leo jijini Dar es Salaam,Meneja Habari na Mahusiano wa NHC,Muungano Saguya wakati akiongea na waandishi wa habari kwa shughuli mbalimbali walizozitekeleza tangu walipoanza mwaka 2021 na mipango waliyona kwa mwaka ujao 2022.

Alisema katika kutekeleza mpango huo,shirika hilo litafata sheria zote ya mpangaji kama kawaida hivyo kama mpangaji  akiwa hajalipa kodi kwa muda unaotakiwa atapatiwa notisi.

“Notisi hiyo ambayo itakuwa ni ya siku 30 baada ya hapo atapewa notisi na dalali wa mahakama ya siku 14 kisha kumalizika kwa utaratibu huo utaratibu wa kumfungia utakuwa umekamilika,”alisema na kuongeza

“Hii itazuia kidogo kwenye suala la ulimbikizaji wa madeni,hii inakuwa kama wanavyofanya watu wa  kwenye umeme na maji,”alisema

Aidha alisema ifikapo mwezi Januari mwakani ,shirika lao  litaanza mpango kabambe la kukusanya madeni yake yote kwa wapangaji walihama na madeni pamoja na waliolimbikiza kodi.

Alisema  maelekezo haya yametolewa na Serikali,Bodi pamoja   na Menejimenti ya shirika hilo kuhakikisha  kodi hizo zinakusanywa kwa watu hao ambao sio waaminifu.

“Kodi hizi zikikusanywa zote zinauwezo wa kujenga nyumba nyingine 450 na kusaidia watanzania wengine kupata makazi,hatutakuwa na msalie mtume kwa mtu ambaye hawezi kulipa kodi,”alisema  na kuongeza

 “Hivi sasa tunachambua madeni haya ni nani ni nani,…na anadaiwa kiasi gani,tujue kama wapo hai au wapo sehemu gani tutashirikiana na Mamlaka zingine Nida na Brella kuhakikisha  tunataarifa zao zote muhimu hasa kwa watu ambao wametelekeza nyumba na kuacha madeni makubwa,”alisema 

Hata hivyo Saguya alisema kwa mwaka 2022 shirika lao linatarajia kutekeleza ujenzi wa majengo ya biashara ya Kashozi mkoani Bukoba,Mtanda mkoani Lindi,Kahama mkoani Shinyanga pamoja na Masasi mkoani Mtwara.

“Shirika pia linatarajia kujenga nyumba za makazi Isomvu Sumbawanga na maghala ya mazao sehemu mbalimbali ya nchini huku kuendelea na mradi wa uuzaji wa viwanda  kwaajili ya ujenzi wa nyumba za makazi na majengo ya biashara,”alisisitiza Saguya

Alisema katika mwaka huo 2022,NHC inatarajia kuanzisha viwanda vyake vya matofali,kokotona bati kwaajili ya kupunguza gharama za ujenzi na kupata vifaa bora vya utekelezaji wa miradi yao.

Meneja Habari na Mahusiano wa shirika la nyumba la Taifa Muungano Saguya akizungumza na waandishi wa Habari.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...