Adeladius Makwega,Dodoma.


Machozi yangu yote namalizika
Mie nitalala na nani
We unaenda
Mie mpaka ni mawazoo ooh ooh

Mie mpaka ni kuwazawaza
We unaenda
Unaenda
Kama ile njia yako enda

Kama ni maisha yako fuata
Wee dada
Rail on
Rail on, rail on, rail on

Think thats the way
Rail on, rail on, rail on
Think thats the way
Leo paka ni mawazo ooh

Hapo unaniacha ohh
Kama we unaenda
We unaenda
We unaenda

Rail on, Rail on, Rail on
Think thats the way
Rail on, Rail on, Rail on
Think thats the way

Rail on, Rail on, Rail on
Think thats the way
Rail on, Rail on, Rail on
Think thats the way.

Rail On.

 

Hayo uliyosoma ni mashairi ya Wimbo Rail On (machozi) wa Jules Shungu Wembedio Pene Kikumba(Papa Wemba) mwanamuziki aliyekuwa na asili ya Kongo ambaye alikuwa akicheza muziki wa Rumba, Soukus na Ndombolo.

Wimbo huu una maneno 102 huku maneno Rail On pekee yakijirudia mara 20 kwa 20 kwa hiyo maneno 62 ndiyo yalitumia lugha ya Kiswahili. Ninaweza kusema wimbo huu umeimbwa Kiswahili kwa msingi wa maneno mengi yalitumika dhidi ya maneno ya kimombo. 

Siku ya jana niliukumbuka wimbo huo ambapo unazungumzia mapenzi wa kiume ambaye analalamika kuondoka kwa mpenziwe wa kike, mtunzi hakueeleza kuwa kama mpenzi wake wa kike amemuacha kwa kwenda kwa bwana mwingine ama ameondoka duniani.

Lakini mkomonzio wa wimbo huo unajengwa katika huzuni kubwa ya mpenzi wa kiume kwa kilio hicho. Muziki unaweza kujengwa katika maneno ukatoa taswira ya wimbo,una weza ukajengwa katika vyombo tu ukaonesha taswira yake na pia hata sura ya yule anayeimba inaweza kuonesha taswira ya wimbo huo. 

Leo hii mwanakwetu naweka kalamu chini hapo, nikikumbusha kuwa Aprili 24, 2022, itakuwa imetimia miaka 6 tangu Papa Wemba afariki dunia.Ndugu huyu ana nyimbo tele kama vile Yolele, Mandola, Show me the way, Shofele na nyingine nyingi.Nakutakiwa siku njema.

 

Makwadeladius@gmail.com

0717649257

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...