Na Said Mwishehe, Michuzi TV

UCHUKUAJI wa fomu za kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  lina zidi kushika kasi  ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo  Kada  wa Chama hicho Joseph Elias Sabuka ni miongoni mwa makada waliochukua fomu  hiyo.

Kada huyo amechukua fomu katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, leo Januari 13,2022 , ambapo ameeleza kuwa  amejitathimini  na kuona  ana uwezo  na Sifa  za kuongoza mhimili huo.

“Uzoefu nilio nao ndiyo utakaonivusha katika mchakato huu kumpata spika. Nikichaguliwa kuwa spika   kitakachoniongoza ni sheria kanuni na miongozo. Nitakuwa imara kuisimamia na kuhakikisha siyumbi.Nitaisamimia Serikali na kuikosoa pale  kwenye ulazima wa kufanya hivyo,” amesema Sabuka.

Kada huyo, ambaye ni Ofisa Mwandamizi katika Serikali ya Awamu ya Sita anayehudumu katika Wizara ya Fedha na Mipango mesema haoni kama kuna shida  kwake  kugombea nafasi hiyo kwani uzoefu  alio nao katika kutekeleza majukumu ya Chama na serikali  ndiyo utakaomvusha katika mchakato huo.

“Ni meamua kugombea kwani ni haki yangu  kikatiba, demokrasia ,  nina sifa,  uwezo  na nia”amebainisha”.

Ameleeza  mwaka 2020 aliwahi kuomba ridhaa  ya Chama kugombea nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kinondoni mkoani Dar es Salaam lakini kura hazikutosha na sasa ameona  ni wakati  sahihi kwake kuomba kuwania nafasi ya Spika wa Bunge.

Amezungumzia pia mfumo wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu ndani ya CCM  ambapo ametoa pongezi kwa chama chake kwan namna  ambavyo  utaratibu  uliowekwa ni rafiki na wa kidemorasia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...