Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

Jeshi la polisi makao makuu limefanya uzinduzi wa matumizi ya mashine mpya za malipo kwa ajili kukusanya maduhuli ya serikali katika mkoa wa kipolisi Rufiji kwa kamanda wa polisi,mafisa,askari wa usalama barabarani pamoja na wahasibu.

Lengo la mashine hizo mpya zenye uwezo mkubwa Sambamba na mafunzo ni kuwajengea uwezo wa kutoa huduma kwa muda mfupi na kuondoa malalamiko yaliyokuwa yakijitokeza kipindi cha nyuma.

Hayo yalisemwa na Kamishna msaidizi wa jeshi la polisi Leonard Ngassa alipofanya ziara katika mkoa wa kipolisi Rufiji ,kutoa elimu kwa askari juu ya matumizi ya mashine mpya za kukusanya maduhuli ya serikali.

Alieleza, mashine hizi zitakuwa na uwezo mkubwa tofauti na awali kwani zimeongezewa baadhi ya mifumo ili kutoa huduma kwa haraka.

"Nia ya ziara yetu ni kutoa elimu na uzinduzi wa matumizi ya mashine hizi,Tunaishukuru Serikali kwa kuliwezesha Jeshi la polisi kwa ajili ya ununuzi wa mashine hizo, Tutaanza kutoa mafunzo nchi nzima kwa makamanda wa polisi,askari wa usalama barabarani, maafisa,wakaguzi na wahasibu" alifafanua Leonard Ngassa-Kamishna msaidizi wa polisi kutoka makao makuu.

Nae Kamishna msaidizi wa jeshi la polisi na Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Rufiji ,Kungu Malulu alisema mashine hizo zitaongeza ufanisi wa kazi kwa askari pamoja huduma bora kwa wananchi wa mkoa wa kipolisi Ruiji.

"Tumepokea ugeni kutoka makao makuu kwa Ajili ya askari wetu ambapo pia tumepokea mashine hizi za kisasa"

Malulu alibainisha,kwa hakika ujaji wa mashine hizo utaboresha utoaji huduma na kuongezea ufanisi wa kazi kwa askari Rufiji na maeneo mengine.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...