SERIKALI ya Tanzania inashiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Utalii (FITUR) yanayofanyika katika ukumbi wa IFEMA mjini Madrid, Uhispania.

Tanzania inawakilishwa na  Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa wenye kuwakilisha  Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania pia katika Falme ya Uhispania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (United Nations World Tourism Organisation), Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Eneo la Hifadhi la Ngorongoro (NCCA), Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA) na Mamlaka ya Huduma za Misitu (TFS).

Lengo la maonyesho hayo ni kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika nchi washiriki ili kuinua sekta ya utalii.Maonyesho hayo yalifunguliwa jana tarehe 19 Januari 2022, na Mfalme Felipe VI, ambayo yatahitimishwa tarehe 24 Januari 2022.

Banda la Tanzania limekuwa kivutio kwa kutembelewa na wageni wengi ambao wameonyesha nia ya kutembelea Tanzania bara na visiwani. Maonyesho hayo yanashirikisha nchi zaidi ya 160 na kuhudhuriwa na mawaziri kadhaa wa Utalii kutoka nchi mbalimbali duniani.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...