Na Mwandishi wetu, Simanjiro

KIKUNDI cha Faraja cha Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kimekarabati darasa moja la shule ya msingi Mirerani kwa gharama ya shilingi milioni 1.6.

Katibu wa Faraja, Lidya Mollel akisoma taarifa wakati wa kukabidhi darasa hilo kwa Diwani wa kata ya Endiamtu Lucas Zacharia amesema waliamua kulikarabati kama hisani kwa jamii.

Mollel amesema ili kuunga mkono jitihada za dhati za Rais Samia Suluhu Hassan ya ujenzi wa madarasa katika shule mbalimbali hapa nchini nao wakaiga jambo hilo la maendeleo.

Amesema kikundi hicho huwa wanakutana mara moja kwa mwezi kwenye shule hiyo ndiyo sababu wakakarabati daraja moja la shule hiyo ya msingi Mirerani.

Amesema ukarabati uliofanyika ni kuweka sakafu, kupiga plasta ndani sehemu zote zilizobomoka, kupiga puchi ya nje na ndani, ukuta wa ndani wa darasa hilo na kupiga rangi ndani.

“Tunamshukuru mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mirerani Tunisia kwa ushirikiano aliotupatia na kukubali ombi letu la kuruhusu kufanyia vikao hapa shuleni,” amesema Mollel.

Diwani wa kata ya Endiamtu Lucas Chimba Zacharia amewapongeza wanachama wa kikundi cha Faraja kwa kufanikisha ukarabati wa darasa moja la shule ya msingi Mirerani kwa gharama zao.

“Ninawashukuru na kuwapongeza wanachama wa Faraja kwa kuamua kuiunga mkono Serikali na kukarabati darasa moja ambalo lilikuwa linawapa wakati mgumu wanafunzi kusoma,” amesema Luka.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mirerani Tenisia Katukuru aliwapongeza wanachama wa Faraja kwa kukarabati darasa hilo moja la shule yake kwani hivi sasa wanafunzi wanasoma vizuri.

“Awali darasa hilo lilikuwa limechakaa hata kuvuta dawati ilikuwa shida kwani kulikuwa na mabonde mabonde hivyo wanafunzi kutokuwa na wasaa mzuri wa kusoma,” amesema.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...