Na.Khadija Seif, Michuzi TV
ALBUM fupi ya MSANII wa Bongofleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond platinum iliyobeba takribani Nyimbo 10 yasikilizwa Kwa mara ya kwanza katika ukumbi wa Terrace slipway jijini Dar es salaam.

Album hiyo iliyobebwa na jina la "Foa" imepokelewa na kuhudhuriwa na Mastaa mbalimbali ndani na nje ya nchi akiwema Msanii Shodmajozi kutoka Afrika kusini.

Katika Nyimbo hizo 10 ameweza kushirikisha wasanii kama Zuchu,Mbosso, shodmajozi na Focalist kutokea nchi Afrika kusini.

Aidha, vibao vinavopatikana kwenye album fupi hiyo ni Nawaza,okoa,Wonder,Fresh,Sana,Mtasubiri,Fine, Somebody pamoja na Melody ambapo Kwa Sasa inapatikana kwenye Mitandao yote ya kupakua Muziki.
Diamond platinum pamoja na Zuchu wakitumbuiza pamoja baada ya kutambulisha wimbo "Mtasubiri" walioshirikiana katika Album fupi "FOA" iliyoachiwa rasmi katika ukumbi wa Terrace slipway jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...