Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewaagiza Makamanda wa Polisi nchi nzima kufanya operesheni ya mwezi mmoja ya kudhibiti makosa ya usalama barabarani ambayo kwa kipindi cha mwezi wa tatu mwaka huu yameonekeana kuongezeka.

IGP amesema hayo jijini Dar es salaam wakati akizungumza kwenye kikao kazi na Makamanda wa Polisi wa mikoa ya Dar es salaam, Morogoro, Pwani, Rufiji ma RTOs na DTOs pamoja na Wakuu wa Operesheni kutoka kwenye mikoa hiyo.

Aidha, katika kikao kazi hicho IGP Sirro ametoa agizo kwa wananchi kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani kwa lengo la kuepusha ajali zinazoweza kuepukia.

Katika hatua nyingine IGP Simon Sirro amekutana na kuzungumza na balozi wa Palestina nchini Tanzania Mhe. Hamdi Mansour Abuali aliyemtembelea ofisini kwake Makao Makuu Ndogo ya Jeshi hilo na kujadiliana mambo mbalimbali kuhusiana na masuala ya usalama na ushirikiano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...