Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa Cde. Victoria Mwanziva ashiriki Darasa la itikadi Tawi la UVCCM Msakuzi Mashariki- Kata ya Mbezi- Wilaya ya Ubungo- Mkoa wa Dar-Es-Salaam.
Cde. Victoria Mwanziva amewafunda vijana wa Hamasa katika darasa la Itikadi lilioandaliwa na Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Msakuzi; akiwasihi kujidhatiti ya kwamba hamasa ya kukipigania Chama huanzia ngazi ya Tawi; kwani huko ndiko kwenye wanachama wengi.
Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa Cde. Victoria Mwanziva amewasihi Vijana wote wa UVCCM; Kuendelea kutembea kifua mbele kusemea mambo mazuri na makubwa yanayofanywa na Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa taifa letu la Tanzania.
Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa Cde. Victoria Mwanziva aliambatana na Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Mkoa wa Dar-Es-Salaam Cde. Eng Ally Ummiy- na Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Mbezi Mary Biita
katika tukio lililoandaliwa na Mwenyekiti wa UVCCM Tawi la Msakuzi Mashariki Cde Noel Kapinga ambaye alikuwepo na viongozi wa Tawi na Kata wa Chama na Jumuiya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...