Familia ya Emmanuel Ole Naiko inasikitika kutangaza kifo cha BABA YAO, BALOZI EMMANUEL OLE NAIKO kilichotokea leo 30/03/22, nyumbani kwake Bahari Beach, Dar es Salaam.
Habari ziwafikie wana familia waliopo Dar es Salaam, Monduli-Arusha na kwengine kote.
Balozi Ole-Naiko amewahi kushika nyadhifa mbali mbali kwenye serikali ikiwemo Mkurugenzi mkuu wa kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
Wakati wa mauti unamfika alikuwa ni balozi wa Heshima wa Botswana.
Mipango ya mazishi inaendelea nyumbani kwake Utulivu Road, Bahari Beach, Dar es salaam
Bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.
2 Timotheo 4; 7
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...