Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema kuwa, uhalifu nchini umeendelea kudhibitiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na jitihada mbalimbali na ushirikiano wa vyombo vya ulinzi na usalama, vikundi vya ulinzi shirikishi pamoja na wananchi.

IGP Sirro amesema hayo akiwa wilaya ya Urambo na Kaliua mkoani Tabora ambapo pia ameelezea changamoto za mauaji ya ushirikina na kuwataka wananchi kuachana na imani potofu na zilizopitwa na wakati na kwamba Jeshi la Polisi litaendelea kuwachukulia hatua kali watu wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Aidha IGP Sirro amevitaka vikundi vya ulinzi shirikishi kuzingatia sheria na kuwahudumia wananchi badala ya kuwa kero kwa wananchi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya vijana wa vikundi vya ulinzi shirikishi wilaya ya Urambo mkoani Tabora baada ya kumaliza mkutano wa hadhara na wananchi ambapo IGP Sirro aliitaka jamii hiyo kuachana na vitendo vya mauaji vinavyotokana na imani za kishirikina, wizi wa mifugo pamoja na vitendo vya ubakaji. Picha na Demetrius Njimbwi wa Jeshi la Polisi
 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...