CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimepiga marufuku wagombea nafasi za uongozi ndani ya Chama hicho nchi nzima ambao ni viongozi kutojihusisha kwenye  kutoa fomu za kugombea uongozi au kusimamia Uchaguzi.

Kimesema iwapo kiongozi kwenye nafasi yoyote anagombea nafasi ndani ya Chama hicho ni vema Chama kikateua mtu mwingine wa kusimamia ili kuhakikisha haki inatendeka katika mchakato wa Uchaguzi unaoendelea nchi nzima.

Hayo yamesemwa na  Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo alipokuwa kwenye ziara yake mkoani Shinyanga ambapo amezungumzia umuhimu wa kutenda haki kwenye mchakato huo wa Uchaguzi.

Amefafanua kwamba  mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi ndani ya chama,  hivyo wagombea ambao kwa sasa ni viongozi ngazi zote hawapaswi kusimamia uchaguzi ili hali wao ni sehemu ya wagombea na kutaka wakae pembeni kuanzia mchakato wa awali wa ugawaji wa fomu, mpaka vikao vya kupitisha wagombea ili kuwepo na uchaguzi wa haki.

Ameongeza  fomu zitolewe kwa wogombea wote na pale ambapo kiongozi yoyote ndani ya chama anawania nafasi ni marufuku kuhusika kwenye mchakato wa uchaguzi, wabaki kuwa wagombea kama wanachama wengine ili haki itendeke, na hii ni kwa nchi nzima.

"Kama Katibu wa ngazi husika anagombea kamati ya siasa ichague mjumbe mmoja miongoni mwa wajumbe asimamie uchaguzi, na kama Kamati nzima ya siasa inagombea, ngazi ya juu iteue kiongozi mmoja asimamie uchaguzi huo ili kujiepusha na ujanja ujanja wa baadhi ya viongozi wagombea kuficha fomu kwa baadhi ya wagombea wenzao  kwa maslahi yao binafsi badala ya chama,"amesema Chongolo.

Pamoja na kupiga marufuku hiyo , Chongolo amepata nafasi ya kufafanua kwa kina namna ambavyo wanachama wa Chama hicho kwa ngazi mbalimbali kuendelea kushirikiana na viongozi na Wananchi kwa ujumla kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali kwa niaba ya CCM.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...