Mamlaka
ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeshiriki katika maadhimisho ya
wiki ya ununuzi wa Umma kwa kutoa elimu kwa wananchi kupitia maonesho
yaliyofanyika katika viwanja vya AICC jijini Arusha.
Maonesho
hayo ni sehemu ya wiki hiyo ya manunuzi yenye kauli mbiu ya ‘Matumizi
ya teknolojia katika kubiresha ununuzi wa umma’ ilizinduliwa Alhamisi
tarehe 5 Mei 2022 na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa (Mb)
jijini Arusha.
Afisa
mtoa taarifa za Usafiri wa Anga Mwandamizi kituo cha Mamlaka ya Usafiri
wa Anga Tanzania (TCAA) Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro
(KIA) Bw. Paul Mrema akitoa maelezo ya namna ndege inavyopatiwa
taarifa muhimu kabla ya kuanza safari kwa mwananchi aliyefika kwenye
banda la TCAA ambapo Mamlaka inashiriki wiki ya ununuzi wa umma
inayoadhimishwa Arusha katika ukumbi wa AICC (wakwanza kulia) ni Afisa
Muongozaji ndege wa TCAA kituo cha Uwanja wa ndege wa Arusha Bw. Mgaza
Emmanuel.
Afisa
Habari wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Ally Changwila
akitoa elimu kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha waliofika kwenye banda la
maonesho ya TCAAambapo Mamlaka inashiriki wiki ya ununuzi wa umma
inayoadhimishwa Arusha katika ukumbi wa AICC.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...