Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema serikali imeendelea kuhimiza makusanyo ya fedha za Umma yafanyike kwa kutumia mfumo wa kielektroniki ikiwa ni utaratibu wa kudhibiti upotevu wa fedha na kuongeza mapato.

IGP Sirro amesema hayo akiwa jijini Dodoma wakati akifungua kikao kazi cha Wakuu wa vituo tiba vya Jeshi la Polisi ambapo kikao kazi hicho kitafanya tathimini ya utendaji kazi na kuibua mapungufu sambamba na kujadili changamoto mbalimbali kwa ajili ya kuleta tija mahala pa kazi.

Aidha, IGP Sirro ameongeza kuwa ni vyema hospitali za Jeshi hilo zikawa kimbilio la wananchi wote kwa kutoa huduma bora kwa wateja.

Naye Mkuu wa Kikosi cha Afya Nchini Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Hussein Yahaya amesema kuwa, hadi sasa kuna jumla ya vituo tiba 36 nchini ambavyo vimeendelea kutoa huduma mbalimbali za kitabibu na kwamba licha ya kuhudumia afya za askari na familia zao lakini pia wameendelea kutoa huduma za afya kwa wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...