Na Mwamvua Mwinyi,Pwani


Mashirika yasiyo ya kiserikali, Mkoani Pwani yamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan  Kwakupewa ushirikiano na mazingira mazuri ya kuweza kutekeleza Miradi mbalimbali katika jamii.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Direct Aid Dr.Adam Othman wakati wakizindua mradi wa kituo Cha elimu Cha taasisi ya wasioona ya Waisalmu ya (VIMDAT) katika Kijiji Cha Mwanambaya mkuranga mkoani Pwani

Aidha sheikh wa Mkoa Pwani alhaji khamisi Mtupa alizikumbusha mamlaka kuwatendea wema wenye Uhitaji nchi kupata tahfifu ya Mungu.
awali akisoma Risala Mwl.Musa njechele ametaja Changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo Uhitaji wa Miundombinu ya Barabara Umeme na Maji.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani ,Abubakar Kunenge ameziasa Taasisi hizo licha ya kuwajengea miundombinu na kuwapa taaluma pia wawazeshe walemavu hao  waweze kujiingizia kipato na kujitegemea

Akitoa shukrani Rais wa Taasisi ya wasioona ya Waisalmu (VIMDAT) amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan Kwa Uongozi wake uliotukuka unao wajali watu walemavu pia.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...