Na John Walter-ManyaraShirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa kushirikiana na jeshi la polisi mkoani Manyara limeanza operesheni ya kuwabaini wezi wa miundombinu ya umeme ambapo Watu saba wamekamatwa katika wilaya ya Babati.

Kaimu Meneja wa TANESCO Mkoa wa Manyara Mosses Kisanza amesema walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kwamba katika kijiji cha Shaurimoyo waya katika nguzo 13 zimekatwa na watu wasiojulikana.

Aidha waligundua mradi uliojengwa kinyume na taratibu za shirika hilo (ILLEGAL) katika kijiji cha Kiru Six wilayani Babati ambapo zimejengwa nguzo tano na kuunganisha waya zikisubiri kuwaunganishia wateja.

Kisanza amesema katika operesheni hiyo walibaini uharibifu kufanywa katika nguzo kubwa (Gridi ya taifa) 220KV kutoka kituo cha kupooza Umeme cha wilaya ya Babati kwenda Arusha ambapo kuna baadhi ya vyuma vimefunguliwa kwenye nguzo zilizopo katikati ya Minjingu na Mbuyu wa Mjerumani.

Katika hatua nyingine Kisanza amewaomba wananchi na wasamaria wema kushiriki katika kutoa taarifa za siri ambazo zitafanikisha kuwakamata wananchi wanao hujumu miundmbinu ya umeme.
Hata hivyo shirika la Umeme mkoani Manyara bado linafanya tathmini juu ya uharibu uliofanywa.
Akizungumzia tukio la watuhumiwa hao saba wa miundo mbinu ya TANESCO Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara Benjamin Kuzaga amesema watu hao watafikishwa mahakamani muda wowote upelelezi ukikamilika.

Amesema kwa kushirikiana na TANESCO walifanya msako maeneo mbalimbali ya mkoa wa Manyara ambapo walifanikiwa kukamata baadhi ya vyuma ambavyo vinatumika kwenye miundombinu ya TANESCO kwenye nguzo zake za chuma.

Amesema walivikuta vyuma hivyo katika gereji mbalimbali na vingine katika makazi ya watu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...