Na Mwandishi Wetu

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) , Eric Hamissi Leo amekutana na kufanya Mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa  (CEO)  wa Shirika kubwa la Meli la Linear Messina Duniani  lenye makao makuu Italy Ndugu Ignazo Messina katika ofisi za Bandari Jijini Dar es Salaam.

Katika ugeni huo Mkurugenzi wa Messina  amemkabidhi  tuzo  ya ushirikiano Mzuri baina ya TPA na Messina.

Ndugu Ignazo amefurahishwa na utendaji kazi mzuri wa TPA na ameahidi kushirikiana zaidi na TPA MESSINA ili Kuongeza Idadi ya meli zitakozoingia bandari za Tanzania

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TPA  ndugu ,Eric Hamissi ameahidi kuongeza ushirikiano mzuri na Shirika Hilo ili kuongeza ufanisi katika kuhudumia meli zinazoingia  katika Bandari ya Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...