JAMHURI ya Muungano wa Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano mkubwa wa Shirika la Utalii Duniani ( UNWTO), utakaofanyika mjini Arusha kuanzia tarehe 5 - 7 Oktoba 2022.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Paris  kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii ulikuwa mstari wa mbele kuzishawishi nchi wanachama wa UNWTO kukubali mkutano huo ufanyike  nchini Tanzania.

 Mkutano huo pamoja na kuwaleta Mawaziri wa Utalii kutoka nchi zote za Afrika, pia utahudhuriwa na wadau wa utalii kutoka nchi mbali mbali duniani wanachama wa UNWTO.

 Aidha, Mkutano huo utaitangaza zaidi filamu ya Tanzania Royal Tour yenye lengo  la kukuza sekta ya Utalii na kuvutia uwekezaji katika sekta hiyo. Juhudi hizo ni utekelezaji wa maagizo ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu kujikita katika utalii wa mikutano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...