Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Albert John Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam Agosti, Mosi, 2022.

Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuasa Mkuu wa Mkoa mteule wa Kagera, Albert John Chalamila kuacha utundu katika majukumu ya uongozi katika nafasi anazoteuliwa na Mamlaka.

Rais Samia ameyasema hayo, Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akiwaapisha Viongozi hao aliowateua hivi karibuni, Mhe. Samia amesema RC Chalamila ni mfanyakazi mzuri lakini utundu ndio unamsumbua.

“Natumaini sasa umekuwa na akili imetulia sasa, natumaini utanisaidia kwenye masuala mbalimbali lakini bado nakuangalia kwa karibu sana.”Amesema Mhe. Rais

“Wananchi wakija na Mabango, maana yake Wananchi wanalalamika, Mwananchi akija na Bango ujue analalamika. Mimi nilikataa Mabango ili ninyi Viongozi niliowateua mkafanye kazi vizuri bila Wananchi kulalamika, nataka muende kuwahudumia Wananchi.” Ameeleza Mhe. Rais.

Katika uapisho huo wa Viongozi wateule, Rais Samia amewaapisha Wakuu wa Mikoa tisa kwa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa saba, pia wapo Wakuu wa Taasisi na Mashirika mbalimbali tisa ambao amewateua hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...