Wanging’ombe

Mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe mkoani Njombe Lauteri Kanoni ameagiza wakuu wa shule na maafisa elimu katika wilaya hiyo kuwasimamia wasaidizi wao (walimu) wasiweze kutoroka kwenye vituo vyao vya kazi wakati wa muda wa muajiri wao na kwenda kutafuta fedha za kujiongezea vipato kwa kuwa serikali imeshatoa fedha kwa ajili yao.

Ametoa agizo hilo wakati akizindua vitabu vya mwongozo wa kufundishia na ujifunzaji kwa walimu na wanafunzi ambapo amesema kuwa Bado kuna changamoto ya utoro kwa wanafunzi na walimu.

“Sio utoro tu kwa wanafunzi upo utoro na kwa walimu kwa hiyo maafisa elimu,wakuu wa shule mkawasimamie wasaidizi wetu wasitoroke watimize dajibu wao,sasa hivi serikali imeshamwaga mahela tena wala sio ya UVIKO ila ni ya kwetu sisi wenyewe”amesema Kanoni

Vile vile ameelekeza shule zilizopewa jukumu la kujenga madarasa ziweze kuanza kufanya maandalizi ya kutosha kwa kuwa tayari serikali imetoa siku 75 kwa wakuu wa mikoa,wilaya na wakurugenzi.
Mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe Lauteri Kanoni akizungumza na Mwalimu pamoja na wanafunzi katika ukumbi wa halmashauri hiyo wakati akizindua vitabu vya mwongozo wa kufundishia na ujifunzaji kwa walimu na wanafunzi
B:Mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe,mkurugenzi wa halmashauri Bi,Mariamu Mhaji wa kulia pichani wakikata utepe kuashiria ishara ya uzinduzi itabu vya mwongozo wa kufundishia na ujifunzaji kwa walimu na wanafunzi wilayani humo.
Baadhi ya Mwalimu na wanafunzi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...