NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MBEYA

WALIMU nchini wamehimizwa kuweka amana zao kwenye benki ya Mwalimu Commercial Bank Plc. Ili waweze kupata manufaa zaidi.

Hayo yamesemwa na Kaimu rais wa Chama cha Walimu nchini, Mwalimu Dinna Mathamani kwenye Mkutano Mkuu wa sita wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Mbeya Alhamisi Oktoba 6, 2022.

“kwa sisi wana hisa tunaona mwelekeo mzuri wa benki yetu, mimi kama kiongozi wa Chama cha Walimu nawahimiza walimu kuendelea kuweka amana zao kwenye benki yetu ili tuendelee kupata manufaa zaidi.” Alisema.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu wa CWT, Mwalimu Maganga Japhet alisema wao kama chama wamekuwa bega kwa bega na benki na kwa sasa watumishi wote wa chama wanapitishia mishahara yao kwenye benki ya Mwalimu Commercial Bank.

“Walimu wana hisa asilimia 35.29%  hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunaiimarisha benki yetu na ili kufikia malengo ya kuanzishwa kwake.” Alifafanua Mwalimu Japhet.

Awali Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Mwalimu Commercial Bank Plc. Francis Cecil Ramadhani amewapongeza wanahisa wote kwa hatua ambayo benki imefikia kwa sasa, kwani kuanzia Julai mwaka jana benki imeanza kutengeneza faida mwezi hadi mwezi.

“Benki pia imeweza kukuza thamani ya mali zake kwa asilimia 53% na kufikia shilingi za Kitanzania Bilioni 58 kutoka shilingi Bilioni 38.” Alifafanua Ramadhani.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc. Richard Makungwa, amewahakikishia wanahisa na wateja wa benki hiyo kuwa benki imeendelea kuimarisha mifumo ya kidijitali (TEHAMA), ambapo mteja anaweza kupata huduma za kibenki akiwa mahala popote kwa kutumia simu ya kiganjani *150*31# au MwalimuBank App, Mwalimu VISA card au MwalimuWaka.

“Nipende kusema walimu ni mojawapo ya kundi la wateja wazuri sana najua wenzetu wanawawinda, sisi pamoja na udogo wetu tunaweza kushindana na wenzetu walio katika soko, nitumie fursa hii kuwahimiza walimu karibuni, rudini nyumbani, nyumbani kumenoga ili muone faida na maana ya ninyi kunzisha chombo chenu cha kifedha ambacho nia ilikuwa ni kuwakwamua kiuchumi.” Alihimiza Makungwa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Mwalimu Commercial Bank Plc. Bw. Francis Cecil Ramadhani (aliyesimama) akiwahutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa sita wa wanahisa wa benki hiyo uliofanyika Oktoba 6, 2022 jijini Mbeya.

Afisa Mtendaji Mkuu, Mwalimu Commercial Bank Plc. Richard Makungwa (kushoto), akifafanua baadhi ya mambo wakati wa Mkutano Mkuu wa sita wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa Royal Tughimbe jijini Mbeya Oktoba 6, 2022









 






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...