
Kutoka kushoto ni Kamishna Ardhi Msaidizi Mkoa wa Pwani Hussein Sadiki Idd akiwa na Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kitaifa (SACF) Puyo Nzalayaimisi wakiwa kwenye maonesho yanayoendelea Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.
Mrakibu Kamanda Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Pwani Jeniffer Shirima akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani kwenye mkutano uliofanyika kwenye Maonesho ya tatu ya Uwekezaji na Biashara Mkoa wa Pwani.
Kamishna Msaidizi Ardhi Mkoa wa Pwani Hussein Sadiki Idd akimkabidhi Kamishna Msaidizi ,Msemaji wa Jeshi la Zimamoto Puyo Nzalayaimisi hati ya kiwanja Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.
Na Khadija Kalili, KIBAHA
WAWEKEZAJI wa ndani na nje ya nchi wametakiwa kupitisha ramani za majengo yao katika Ofisi za Makamanda wa Zimamoto kwa kila Mkoa ili kupata ushauri utakaosaidia kulinda usalama zaidi pale panapotokea majanga ya moto na kuathiri uwekezaji wao kazi.
Yamesemwa hayo leo na Msemaji wa Jeshi la Zimamoto Kitaifa Kamishna Msaidizi Muandamizi (SACF) Puyo Nzalayaimisi (SACF) alisema hayo alipotembelea kwenye banda la Zimamoto katika maonesho ya Wiki ya Uwekezaji na Viwanda Mkoa wa Pwani ambayo yanaendelea katika Viwanda vya Stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani.
Amesema lengo haswa la kushiriki kwenye maonyesho hayo ni kutoa elimu kwa umm huku akiwahakilishia wawekezabi kwamba Tanzania iko salama dhidi ya majanga ya moto huku akitoa rai ya kuwataka kupitisha ramani za majengo yao kabya kuwekeza.
Aidha katika hatua ingine Kaimu Kamishna Ardhi Msaidizi Mkoa wa Pwani Hussein Sadiki Idd amekabidhi hati ya umiliki wa ardhi kwa Zimamoto iliyopo katika eneo la Halmashauri ya Chalinze yenye ukubwa wa meta za mraba 317 ambapo watajenga ofisi zake.
"Natoa shukrani za dhati kwa Wizara ya ardhi kwa kutambua unyeti wetu kwa jamii na kutupatia hati ya kiwanj hivyo suala la ujenzi tutalifikisha katika ngazi ya juu ambako ndiko watakakotekeleza.
Mrakibu Kamanda Zimamoto Mkoa wa Pwani Jeniffer Shirima alisema kuwa Mkoa umekua ukitoa mafunzo katika Wilaya zake kwa jamii kuhusiana na kuchukua tahadhari za majanga ya moto ikiwa ni pamoja kusimamia ujenzi wa mpangilio katika sehemu za makazi ya watu na biashara kwa ujumla.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...