Na Mwandishi Wetu
Timu ya taifa ya Iran imeamka katika Michuano ya Kombe la Dunia baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wales katika mchezo wa mzunguko wa pili wa Kundi B uliopigwa kwenye dimba la Ahmad Bin Ali nchini Qatar.
Katika mchezo huo uliokuwa wa kasi muda wote mabao ya Iran yamefungwa na Rouzbeh Cheshmi dakika ya 90+8' na Ramin Rezaeian kwenye dakika ya 90+11'. Mabao yote yamefungwa na Wachezaji wenye asili ya Ulinzi wakiwa uwanjani.
Iran walipoteza mchezo wao wa mzunguko wa kwanza wa Michuano hiyo baada ya kufungwa mabao 6-2 dhidi ya timu ya taifa Uingereza, huku Wales wakipata sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya taifa ya Marekani.
Msimamo wa Kundi hilo, Uingereza anaongoza akiwa na alama sita akiwa na mchezo mmoja pekee, huku Irani nafasi ya pili wenye alama tatu wakiwa na michezo miwili, Marekani nafasi ya tatu na alama moja sawa na Wales. Uingereza anakutana na Marekani katika mchezo wa mzunguko wa pili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...