Na.Khadija Seif,Michuzi TV
MJADALA wa Kitaifa wa Nishati safi ya kupikia umefunguliwa rasmi leo November Mosi Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) n kwa siku 2 ikiwahusisha wadau,taasisi mbalimbali kwa lengo la kujadili matumizi ya Nishati safi ya kupikia.
Akizungumza
 jijini Dar es salaam leo Novemba mosi Katibu Mkuu wizara ya Nishati  
Felchesmi Mramba amesema tukio la mjadala huo unafanyika mikoa 
mbalimbali  ikiwemo Tabora,Shinyanga, Iringa,Dodoma na Morogoro huku 
takribani mamilioni ya watanzania wakifatilia kupitia televisheni na 
mitandao ya kijamii.
Aidha,
 Mramba ameeleza kuwa mjadala huo ni safari ya awali ya kuhama kwenye 
nishati isiyo salama ya kupikia na kuelekea nishati safi ya kupikia .
"Tunatambua
 madhara yanayopatikana kwa kutumia nishati ya kupikia isiyo salama na 
inaleta madhara mbalimbali ikiwemo athari kiafya,kiuchumi,kijamii hivyo 
wadau na taasisi zitajadili namna ya taifa litahamia kwenye nishati safi
 ili kuepuka matatizo yanayopatikana kwani waathirika ni vielelezo tosha
 kuwa changamoto bado zinaendelea na jamii bado haijapata uelewa wa 
namna ya kukabili changamoto za nishati isiyosalama.
Hata hivyo mjadala huo umehusisha  wadau,taasisi na viongozi mbalimbali  kiserikali  pamoja na viongozi wastaafu. 
Pia
 Mramba amefafanua kuwa kuwepo kwa mjadala huu wa siku 2 ni ishara ya 
wazi kuwa lengo la kumtua mama kuni kichwani litapata Suluhisho.
Mtaalam
 mwandamizi wa maswala ya Fedha katika shirika la umoja wa mataifa wa 
mitaji ya Maendeleo (UNCDF) Immanuel Muro akichangia mjadala wa 
kupatikana kwa Suluhisho la kitaifa la Nishati safi ya kupikia na 
kueleza kuwa bado asilimia kubwa jamii  haina elimu ya kuelewa madhara 
yanayopatikana katika nishati isiyo salama ya kupikia na kuepelekea 
matumizi ya mkaa na kuni kuendelea kwa baadhi ya jamii.
Hata
 hivyo Muro amesema kuwa ukosefu wa maji safi katika mkoa wa Dar es 
salaam inawezwa kusababishwa na kukatwa kwa miti na misitu kwani mikoa 
ya Lindi,Mtwara, Morogoro ndio mikoa inayotiririsha Maji kufika mkoa wa 
Dar es salaam .
"50%
 ya wakazi wa Dar es salaam wanatumia mkaa kam nishati ya kupikia  
ambapo miaka mitano ijayo changamoto za kiafya zitazidi pamoja na 
changamoto ya kimazingira itakbiliwa na ukame."
Pia
 ametoa rai kwa Serikali kutafuta ufumbuzi  wa haraka na kuhakikisha 
jamii inapata uelewa na kutambua madhara yanayosababishwa na matumizi ya
 Nishati ya mkaa na kuni.
Kwa
 upande wake waziri mstaafu na Mkurugenzi mkuu mstaafu wa shirika la 
umoja wa mataifa wa Makazi duniani (UN_Habitat) Anna Tibaijuka amesema 
yeye ni mmoja ya mashuhuda wa watumiaji wa nishati ya kupikia ya kuni na
 kukiri kuwa ametembea porini kutafuta kuni.
"Tuzungumze
 mkakati wa kitaifa wa kuondokana na kuweza kupikia Nishati safi kiwe 
kikao cha mkakati. Mpangilio ni nzuri na wale walio kwenye TV wanaona 
kwamba Serikali yetu ina mpango Kwa kutusaidia akina mama."
Aidha,Tibaijuka
 ametoa rai kwa  serikali kuweka mkakati wa sera ya kitaifa ya kuweka 
bei isiyobadilika badilka,mpango huu using kuwa kama Agizo tu Bali liwe 
na mpango, sera na mazingira wezeshi kwa watu kumudu gharama hizo.
Mtaalam mwandamizi wa maswala ya Fedha katika shirika la umoja wa mataifa wa mitaji ya Maendeleo (UNCDF) Immanuel Muro Akizungumza juu ya umuhimu wa Nishati Safi na namna Mkaa unavyochangia kuharibu Mazingira
Mkurugenzi wa Taifa Gesi, Hamisi Ramadhani akichnagia katika Mjadala wa Kitaifa waNishati Safi ya Kupikia .uliofungiliwa leo jijini Dar es Salaam .
Waziri wa Nishati ,January Makamba akiongoza Mjadala wa Kitaifa juu ya Masuala ya Nishati Safi uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.


 






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...