Na Mwandishi Wetu,Mafia.

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba nchini (TMDA) imekabidhi msaada wa dawa za binadamu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia zenye thamani ya zaidi ya milioni 6 kwa lengo la kusaidia matibabu ya wananchi wenye uwezo mdogo.

Dawa hizo zimekabidhiwa na Mkaguzi wa Dawa Bw Japhari Saidi kwa niaba ya Meneja wa TMDA Kanda ya Mashariki (Bw Adonis Bitegeko).

Akikabidhi dawa hizo mbele ya Kamati ya Dawa na Vifaa Tiba (CFDC) ya Halmashauri ya Mafia Bw Japhari ameeleza kuwa lengo la kukabidhi msaada huo wa dawa ni kusaidia wananchi wenye uwezo mdogo au wasio na uwezo kabisa kuchangia gharama za matibabu ili nao wapate dawa zenye ubora, usalama na ufanisi uliothibitishwa na TMDA.

"Dawa hizi zinatokana na sampuli zilizobaki baada ya uchunguzi wa kimaabara kukamilika na kufaulu vipimo.Hivyo, Ndugu Mkurugenzi naomba uzipokee ili ziweze kutumika kusaidia matibabu ya wananchi wa Mafia" Alisema Bw Japhari Saidi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mafia, Mwl Kassim Ndumbo ameishukru TMDA, kwa msaada huo na kuwaomba usiwe mwisho bali iwe na muendelezo kwa maslai ya Wananchi wa Wilaya ya Mafia.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...